COVID-19 yahatarisha kufanya elimu kuongeza mgawanyiko badala ya kujenga usawa- UNICEF
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linasema janga la ugonjwa Corona au COVID-19 likiingia mwaka wa tatu, nchi 23 bado hazijafungua shule zao kikamilifu na hivyo kuwaweka watoto milioni 405 katika hatari ya kuacha shule na zaidi ya yote kuongeza pengo la ufahamu duniani badala ya kuchochea usawa.