Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Raia 11 wa Rwanda wakiwemo wapiganaji wa zamani 4 na wategemezi wao wakiwa wamepiga picha ya pamoja katika kituo cha mpito cha Munigi, Goma jimboni Kivu Kaskazini nchini DRC kabla ya kuondoka kurejea nyumbani 24 February 2022.
UN/Eskinder Debebe

Tamu-chungu ya wapiganaji wa zamani kurejea nyumbani Rwanda baada ya mapigano msituni DRC

“Mke wangu niliyempata wakati napigana porini, alijifungua mtoto, sasa nikaona maisha ya kukimbia huku na kule porini na familia hayawezekani tena bora nirudi nyumbani Rwanda nikalee familia yangu.” Ni Mukeshimana Jean-Nepo, mpiganaji wa zamani wa kikundi cha Raiya Mutomboki nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC akizungumza kwa furaha siku ya kurejea nyumbani Rwanda tarehe 24 mwezi Februari mwaka 2022.