Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kumbukumbu za mikutano kwenye Baraza Kuu

Ijumatatu, Baraza Kuu la UM linajadilia ripoti ya Baraza la Maendeleo ya Uchumi na Jamii (ECOSOC); na pia kuzingatia masuala juu ya uhusiano wamashirika ya kikanda na mengineyo na UM. Kadhalika wajumbe wa kimataifa wanafanya mapitio kuhusu ripoti ya KM ya kumbukumbu za majanga ya maangamizi ya halaiki, hususan lile janga la maangamizi ya wafuasi wa dini ya Kiyahudi kwenye Vita Kuu ya Pili. ~

Hapa na Pale

KM Ban Ki-moon ametangaza kumteua tena Liuteni-Jenerali Babacar Gaye wa Senegal kuwa Kamanda Mkuu wa Dharura wa Vikosi vya MONUC kwa miezi sita ijayo. Lengo la uteuzi huo wa Jenerali Gaye ni kukabiliana vyema na matatizo yaliozuka Kivu Kaskazini katika JKK. Jenerali Gaye alikuwa Kamanda Mkuu wa MONUC kuanzia March 2005 hadi Oktoba 2008.