Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

IOM imeripoti milioni 1.7 wamerejea Sudan Kusini

Shirika la Kimataifa kuhusu Wahamaji (IOM) limeripoti kwamba wahamiaji wa ndani milioni 1.7 wamefanikiwa kurejeshwa makwao, kwa khiyari katika Sudan Kusini kufuatia utiaji sahihi wa yale Mapatano ya Jumla ya Amani yaliokamilishwa mnamo mwezi Januari 2005. ~ ~

Hapa na Pale

Charles Vincent, Mkurugenzi wa Ofisi ya Geneva ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) alisema kwenye mahojiano na Redio ya UM ya kwamba shirika linakabiliwa na upungufu wa dola milioni 46 zinazohitajika kidharura kununua tani 33,000 za chakula ili kuhudumia umma ulioathirika na mapigano katika jimbo la Kivu Kasakazini. Alisema tangu mwezi Agosti watu 200,000 walilazimika kuhama makazi katika sehemeu za mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kwa sababu ya kufufuka tena kwa mapigano baina ya majeshi ya Serikali na makundi ya waasi. Kadhalika matatizo ya utapiamlo yameanza kushuhudiwa miongoni mwa watoto wa eneo hilo.