M. Novak ahadharisha tabia karaha ya kufanya mateso kama desturi za kawaida
Mkariri/Mtaalamu Maalumu Huru wa UM juu ya Mateso, Manfred Novak Alkhamisi alihutubia Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la UM ambapo alihadharisha kwamba katika uchunguzi wake wa kimataifa amegundua na kuthibitisha ya kuwa vitendo vya mateso vinaendelea kufanywa desturi za kawaida katika nchi nyingi za dunia.