Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Mwanamke akiwa amembeba binti yake katika kituo cha Wisdom kilichopo eneo la Gurei mjini Juba nchini Sudan kusini baada ya kupigwa na mumewe.
© UNICEF/Albert Gonzalez Farran

Ukatili majumbani ukiongezeka, Katibu Mkuu wa UN ataka sitisho la vitendo hivyo

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa hatua za kukomesha ghasia na ukatili majumbani dhidi ya wanawake na wasichana, kufuatia ripoti kuwa vitendo hivyo vimeshamiri hivi sasa maeneo mbali mbali duniani baada ya serikali kutaka wananchi wasalie majumbani kuepusha kuenea kwa ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19.

Sauti
2'9"