Sasa ni wakati wa msichana- Ripoti
Wakati umefika wa kusema sasa basi na kupatia wasichana wakimbizi fursa ya kwenda shule hadi elimu ya juu ili waweze kujinasua kutoka lindi la umaskini na mateso, imesema ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR iliyotolewa hii leo ikipatiwa jina, #HerTurn.