Ebola sasa iko Butembo, mashariki mwa DRC- UNICEF
Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa la UNICEF linapanua wigo wa operesheni zake za kukabiliana na ugonjwa wa Ebola nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC baada ya serikali kuthibitisha kuwepo kwa wagonjwa wapya wawili kwenye mji wa Butembo, jimboni Kivu Kaskazini.