Nina Imani UN itatatua changamoto zinazoikabili :FIB
Amani na Usalama
Kikosi maalumu kilichoanzishwa na Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC kwa ajili ya kufurusha makundi ya waasi na kujibu mashambulizi (FIB) kinakabiliwa na changamoto nyingi, japo imani ipo kwamba Umoja wa Mataifa utazitatua.
Hayo yamesemwa na Meja Jenerali Alfred Fabian Kapinga, mkuu wa operesheni na mafunzo wa jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ, ambaye yuko hapa New York kuhudhuria mkutano baina ya Umoja wa Mataifa na Tanzania, mdau mkubwa wa FIB.
Kandoni mwa mkutano huo amenieleza mada walizojadili
(MAHOJIANO NA MEJA JENERALI KAPINGA)