Bila mafuta, hakuna mkate: WFP
Hali mbaya inayowakabili mamia kwa maelfu ya Wapalestina huko Gaza inaweza kuwa mbaya zaidi, kutokana na uhaba mkubwa wa mafuta ambao unatishia kusimamisha chakula na shughuli zingine za kibinadamu.
Hali mbaya inayowakabili mamia kwa maelfu ya Wapalestina huko Gaza inaweza kuwa mbaya zaidi, kutokana na uhaba mkubwa wa mafuta ambao unatishia kusimamisha chakula na shughuli zingine za kibinadamu.
Hebu vuta tasirwa, mama akiwabembeleza watoto wake usiku, hofu ya kutengana nao ikija kama kivuli, kujaribu awezavyo kujilinda yeye na familia yake, ili ‘wasiwe kumbukumbu’ hata hivyo, hadithi yetu ni kumbukumbu tu sasa, lakini wakati ujao bado haujaandikwa, nikiamka kesho, nataka hili limalizike, ilinirejee mahali patakatifu, kwenye nyumba yetu.
Miaka 23 baada ya makubaliano muhimu ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa yanayoangazia wanawake, amani na usalama, wanawake na wasichana bado wanabeba mzigo mkubwa wa migogoro na wanabaki na uwakilishi mdogo katika maamuzi yanayohusu mahitaji ya na haki zao.
Akili mnemba imebadili fani ya sanaa na utamaduni kwa njia ambazo ha ikutarajiwa. Hata hivyo mabadiliko hayo ni ya muda mrefu.
Chini ya kilomita moja kutoka Gaza, vibao vya kuengeshean chakula, mafuta, maji, na dawa ni miongoni mwa mamia ya tani za misaada ya kuokoa maisha iliyopakiwa kwenye msafara mrefu wa malori yakiwa yamesimama kwenye upande wa Misri wa kivuko cha mpakani ch a Rafah, huku madereva wakisubiri ruksa ya Israel ili waweze kufikia Wapalestina milioni 2.3 waliozingirwa na walionaswa katika mzozo wa vita vinavyoendelea.
Ni alfajiri na mapema jua likichomoza kisiwani Pemba, pwani ya Tanzania. Baadhi ya wakazi wa kisiwa hiki tayari wako kwenye mitumbwi wanaelekea kuvuna mazao yao.
Umoja wa Mataifa umekuwa ukifanya kazi katika eneo la Mashariki ya Kati muda wote ili kupunguza mzozo wa Israel na Palestina kwa kuwashirikisha wahusika wakuu na kutoa msaada wa dharura kwa raia walioko mashinani.
Wakati mzozo huo ukiongezeka huku kukiwa na ongezeko la ghasia, kizuizi kamili cha chakula, maji, na huduma muhimu kiliwekwa na Israel huku ripoti zikiibuka kuhusu operesheni za ardhini za Israel huko Gaza, ambako kuna wakazi zaidi ya milioni mbili.