Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au coronavirus">COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19 imedhihirisha umuhimu wa ICT duniani:Guterres
Janga la mlipuko wa virusi vya Corona au COVID -19 limedhihirisha umuhimu wa teknolojia ya Habari na mawasiliano TEHAMA au ICT kwa wasichana na dunia nzima umesema Umoja wa Mataifa.
COVID-19 imepunguza uchafuzi wa hewa lakini sio mbadala wa hatua za mabadiliko ya tabianchi:WMO
Kushuka kwa kiwango cha gesi chafuzi kunakohusiana na mlipuko wa janga la virusi vya corona au COVID-19 ni Habari njema za muda mfupi kwa mujibu wa mkuu wa shirika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO.
Ni lazima tuilinde sayari dunia na watu wake-Guterres
Janga la mlipuko wa virusi vya corona au COVID-19 limefanya macho yote ya Dunia kuelekezwa kwenye mtihani huu mkubwa zaidi ambao ulimwengu umekumbana nao tangu Vita vya Pili vya Dunia amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa
Antonio Guterres katika ujumbe wake maalum wa siku ya kimataifa ya mama sayari Dunia hii leo amesema
22 APRILI 2020
Leo katika jarida la Umoja wa Mataifa Flora Nducha anakuletea
-Umoja wa Mataifa unasema janga la virusi vya Corona au COVID-19 ni kengele ya kuiamsha dunia kuchukua hatua kulinda sayari hiyo na watu wake hasa leo ikiadhimishwa siku ya kimataifa ya mama sayari dunia
- Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF na jiji la Nairobi wanachukua hatua kudhibiti kusambaa wa virusi vya corona au COVID-19, kwenye makazi dunia ya Kibera.
Linapokuja suala la wakimbizi na COVID-19 ni bora kukinga kuliko kuponya:UNHCR
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na wadau wake nchini Bangadesh wanachukua kila tahadhari ili kuhakikisha maelfu ya wakimbizi wa Rohingya kwenye moja ya makazi makubwa kabisa ya wakimbizi duniani ya Cox's Bazaar wanalindwa dhidi ya mlipuko wa Corona au COVID-19.
Janga la COVID-19 ni kumbusho la umuhimu wa sayari dunia:Guterres
Janga la mlipuko wa virusi vya corona au COVID-19 limefanya macho yote ya Dunia kuelekezwa kwenye mtihani huu mkubwa zaidi ambao ulimwengu umekumbana nao tangu Vita vya Pili vya Dunia amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa
Watu 80,000 waathiriwa na mafuriko makubwa DRC
Msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR Andrej Mahecic hii ameviambia vyombo vya habari mjini Geneva Uswisi kuwa UNHCR inashirikiana na mamlaka pamoja na wadau nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kutoa msaada kwa watu 80,000 ambao wameathiriwa na mafuriko makubwa katika jimbo la Kivu Kusini.
21 APRILI 2020
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea
-Mashirika ya Umoja wa Mataifa , EU na USAID wamesema janga la virusi vya Corona au COVID-19 limeweka njiapanda mustakbali wa chakula duniani hivyo hatua zinapaswa kuchukuliwa haraka kuepusha baa la njaa
-Nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR linatoa mafunzo likishirikiana na wadau kuhakikisha wakimbizi wanakingwa dhidi ya COVID-19
Janga la COVID-19 laongeza hatari ya kutokuwa na uhakika wa chakula duniani:EU/UN/USAID
Ripoti mpya iliyotolewa leo na mashirika ya Umoja wa Mataifa, Muungano wa Ulaya na shirika la Marekani la msaada wa kimataifa USAID inaonyesha kwamba janga la mlipuko wa virusi vya corona au COVID-19 linaweka njia panda mustakbali wa chakula na lishe.
UN yatoa ombi kupiga jeki masuala ya kiufundi ambayo ni muhimuli wa vita dhidi ya COVID-19
Wakuu wa mashirika makubwa ya Umoja wa Mataifa ya masuala ya kibinadammu na ofisi mbalimbali leo wamezindua ombo la dharura kwa ajili ya kukusanya dola milioni 350 kusaidia vituo vya kimataifa vya misaada kwa ajili ya watu walio katika hatari zaidi wakati huu wa janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19.