Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Wanufaika wa miradi inayotekelezwa na FAO nchini Somalia
©FAO/Arete/Ismail Taxta

Uwekezaji wa kimkakati unahitajika ili kuboresha uhakika wa chakula na maji kwa mamilioni ya Wasomali

Wakati misaada ya kibinadamu imesaidia baadhi ya maeneo ya Somalia kutotumbukia kwenye baa la njaa, wananchi wa vijiji nchini humo bado wanaendelea kukabiliwa na ukosefu wa uhakika wa chakula limesema shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO hii leo baada ya hivi karibuni kutangazwa matokeo ya uchunguzi wa uhakika wa chakula.