Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN Ethiopia/Getachew Dibaba
Takriban mifugo milioni moja wamekufa kutokana na ukame katika eneo la Somali nchini Ethiopia.

Huu ni ukame mbaya zaidi kuwahi kutokea kwa miaka 40, Mamilioni ya Waethiopia hatarini:UN

Jimbo la Somali lilioko Mashariki mwa Ethiopia limekumbwa na misimu mitatu ya kiwango kidogo cha mvua kilicho chini ya wastani, hali ambayo inazidisha madhila  ya kibinadamu kwa watu wapatao milioni 3.5, ambao ni zaidi ya nusu ya wakazi wa eneo hilo ambao tayari walikuwa katika shida.