Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mwanamke akiwa amembeba mwanaye wakati wa mafuriko mjini Jarkata Indonesia
© WMO/Kompas/Hendra A Setyawan

Mabadiliko ya tabianchi ni tishio kwa binadamu na afya ya dunia , hatua zahitajika sasa:IPCC Ripoti

Ripoti mpya ya jopo la kimataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi IPCC iliyotolewa leo imesema kuchukua hatua sasa dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kunaweza Kuchukua hatua sasa “Kunaweza kulinda mustakabali wetu  kwani mabadiliko ya tabianchi yanayochochewa na shughuli za binadamu yanasababisha usumbufu wa hatari na ulioenea katika mazingira yetu na kuathiri maisha ya mabilioni ya watu kote ulimwenguni, licha ya juhudi zinazofanyika kupunguza hatari hiyo.”