Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN News/Assumpta Massoi

FAO imetuepusha na kilimo cha mazoea- Wanawake Kakonko

Mkoani Kigoma nchini Tanzania hususan katika kata ya Katanga wilayani Kakonko, ushirikiano kati ya serikali na Umoja wa Mataifa kwenye kuhakikisha wakulima wanahimili mabadiliko ya tabianchi umeanza kuzaa matunda. Ushirikiano huo unaosongeshwa na wananchi wenyewe kwa ubia na shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO ni katika kuwapatia wakulima mbinu bora za kilimo ili kuwepo na uhakika wa chakula.

Sauti
4'17"