Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

Mahali unakofanyika mkutano wa Umoja wa Mataifa dhidi ya mabadiliko ya tabianchi COP25 mjini Madrid, Hispania
ifema feria de madrid

Ni muhimu COP25 imalize sintofahamu ya ibara ya sita ya Mkataba wa Paris-Inger Andersen

Mkutano wa 25 wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP25 ukianza hii leo mjini Madrid, Hispania, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Mpango wa mazingira wa Umoja wa Mataifa, UNEP Inger Andersen awali mjini New York Marekani kupitia mahojiano maalumu na UN News amesema moja ya vipaumbele vikuu vya mkutano huu itakuwa ni kufikia muafaka wa ibara ya sita ya mkataba wa Paris ambayo haikupata muafaka katika mkutano wa mwaka jana uliofanyika mjini Katowice Poland.

Sauti
2'4"