Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala ya Wiki

Video screenshot/Loise Wairimu

Kutoka Kenya hadi Marekani kupata mafunzo kwa vitendo

Loise Wairimu, ni msichana ambaye alifunga safari kutoka Kenya kuja hapa jijini New York Marekani katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa ili apate mafunzo kwa vitendo.

Kwa takribani kipindi cha miezi sita amefanya kazi pamoja na timu nzima ya Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa akichota maarifa ya kazi. Loise anaanza kwa kueleza namna safari yake hii ilivyoanza na alichojifunza mchakato huu.

Sauti
6'4"
UN / Anton Uspensky

Umoja wa Mataifa ukitimiza miaka 75 na mafanikio iliyoyafikia

Kesho ni siku ya Umoja wa Mataifa, chombo hicho kikitimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake! Katika mada kwa kina Anold Kayanda anatupitisha safari ya kuanzishwa kwake na zaidi ya yote simulizi ya mtu aliyezaliwa mwaka mmoja na Umoja wa Mataifa, mtu ambaye amewahi kushika nyadhifa ndani ya Umoja wa Mataifa, barani Afrika na ndani ya taifa lake la Tanzania. Kwako Anold!

Sauti
5'24"
WHO/P. Virot

Watu bilioni 1 duniani wanaishi na matatizo ya akili-Takwimu

Kuelekea siku ya afya ya akili duniani itakayoadhimishwa kesho Jumamosi Oktoba 10, takwimu zinaonesha kuwa takribani watu bilioni 1 duniani kote wanaishi na matatizo ya akili. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake kwa siku hii amesema, inabidi hatua zichukuliwe ili kuhakikisha kunakuwa na huduma bora ya afya ya akili kwa wote kwani hivi sasa inaonesha pia kuwa kila sekunde 30 mtu mmoja anajiua kutokana na tatizo hili la afya ya akili. 

Sauti
5'42"