Kutoka Kenya hadi Marekani kupata mafunzo kwa vitendo
Loise Wairimu, ni msichana ambaye alifunga safari kutoka Kenya kuja hapa jijini New York Marekani katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa ili apate mafunzo kwa vitendo.
Kwa takribani kipindi cha miezi sita amefanya kazi pamoja na timu nzima ya Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa akichota maarifa ya kazi. Loise anaanza kwa kueleza namna safari yake hii ilivyoanza na alichojifunza mchakato huu.