Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala ya Wiki

UNnewskiswahili/Patrick Newman

Baada ya kunusurika kifo niliamua kuanzisha taasisi ya kusaidia wajane na mayatima-Bi Kamande

Dianah Kamande ni mama wa watoto wawili nchini Kenya ambaye katika mazingira ya kushangaza, siku moja mume wake alirejea nyumbani akiwa na nia moja tu, kumuua mkewe, wanaye wawili na kisha yeye mwenyewe ajiue. Ingawa watoto walitoroshwa haraka, mama yao hakuwa na bahati hiyo kwani alikatwakatwa kwa mapanga kichwani na sehemu nyingi za mwili hivi sasa zimepandikizwa vyuma na mishipa ya bandia.

Baada ya tukio hilo Dianah amebakia kuwa mjane kwani mume wake alijiua baada ya kufikiri kuwa ameshamuua mkewe.

Sauti
6'22"
© UNICEF/UN045727/Pirozzi

Usafirishaji haramu na changamoto zake Afrika Mashariki

Mapema wiki hii dunia imeadhimisha siku ya kupinga usafirishaji haramu wa binadamu huku Umoja wa Mataifa ukiutaja kama uhalifu mkubwa unaoshuhudiwa katika kila pembe ya dunia. Vita, mabadiliko ya tabicnhi,

umasikini na ubaguzi ni baadhi ya vitu ambavyo vimetajwa kuchochea wasafirishaji haramu kutumia fursa hizo kuendeleza biashara zao za kihalifu. Umoja wa Mataifa unahimiza kwamba juhudi za pamoja ni muhimu katika kusaidia kukomesha uhalifu huo na kuwaadhibu wahusika.Je nchi zinapambana vipi na uhalifu huo? namkaribisha Grace Kaneiya kwa maelezo zaidi

Sauti
5'48"