Usafirishaji haramu na changamoto zake Afrika Mashariki
Pakua
Mapema wiki hii dunia imeadhimisha siku ya kupinga usafirishaji haramu wa binadamu huku Umoja wa Mataifa ukiutaja kama uhalifu mkubwa unaoshuhudiwa katika kila pembe ya dunia. Vita, mabadiliko ya tabicnhi,
umasikini na ubaguzi ni baadhi ya vitu ambavyo vimetajwa kuchochea wasafirishaji haramu kutumia fursa hizo kuendeleza biashara zao za kihalifu. Umoja wa Mataifa unahimiza kwamba juhudi za pamoja ni muhimu katika kusaidia kukomesha uhalifu huo na kuwaadhibu wahusika.Je nchi zinapambana vipi na uhalifu huo? namkaribisha Grace Kaneiya kwa maelezo zaidi
Audio Credit
Assumpta Massoi/ Grace Kaneiya
Audio Duration
5'48"