Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Jarida la Habari

30 Oktoba 2020

Katika kuelekea siku ya miji duniani hapo kesho Oktoba 31, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Abtonio Guterres kupitia ujumbe maalum wa siku hiyo amesema miji imebeba gharama kubwa ya janga la corona au COVID-19 lakini jamii katika miji hiyo zimedhihirisha thamani yake katika kukabiliana nalo.

Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP kwa kushirikiana na serikali ya Kenya leo wamezindua mpango wa ugawaji fedha taslim kwa familia 24,000 mjini Mombasa  katika makazi yasiyo rasmi ambao Maisha yao yamesambaratishwa na athari za janga la COVID-19.

Sauti
10'48"

29 Oktoba 2020

Watoto katika nchi maskini wamepoteza miezi minne ya masomo tangu kuanza kwa janga la COVID-19 yasema ripoti ya UNESCO, UNICEF na Benki ya Dunia.


Virusi visivyojulikana vipatavyo 850,000 viko kwa wanyama na ndege na vinaweza kuathiri binadamu inasema ripoti ya IPBES/CBD 


Ethiopia, kampeni ya kitaifa ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa surua iliyoanza mwezi Juni mwaka huu, imeanza kuonesha mwitikio mkubwa hata miongoni mwa wazazi wa kiume.
 

Sauti
12'29"

28 Oktoba 2020

Filamu yatumika kupambana na ndoa za utotoni na ukatili mwingine wa kingono Sudan Kusini. 


Kutana na mapacha wawili barubaru kutoka nchini Iran, wanasema janga la corona au COVID-19 limewafunza mengi.


Na UNICEF inasema viwango vya unyafuzi Yemen vyavunja rekodi.
 

Sauti
12'12"

26 Oktoba 2020

Ripoti yabaini magari mengi yanayopelekwa nchi za uchumi mdogo hayafai. 
Ukosefu wa ajira na makazi salama vyawaacha wafanyakazi wahamiaji hatarini Lebanon, imesema IOM.
Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO huko nchini Madagascar linatekeleza mradi wa kuhakikisha kuwa wakazi wanaoishi karibu na eneo la hifadhi la Makira wanakuwa na uhakika wa kupata mlo bora bila kusambaratisha eneo hilo la hifadhi.
 

Sauti
12'20"

22 Oktoba 2020

Wadau waandaa mkutano wa kuchangisha fedha kusaidia warohingya.
COVID-19 yaporomosha ununuzi wa nguo duniani, Asia-Pasifiki yaathirika zaidi.
Virusi vya corona vilibadilisha matarajio yangu katika UN lakini nimejifunza SDGs-Loise Wairimu
 

Sauti
12'29"

16 Oktoba 2020

Katika kumulika wito wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa kutaka uwepo wa mifumo himilivu ya kilimo na inayohakikisha upatikanaji wa chakula tunakwenda nchini Tanzania ambako shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO nchini humo linaendesha miradi kadhaa ya kilimo bora na uepushaji upotevu wa mazao kabla na baada ya kuvuna. 

Sauti
10'43"