Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

WFP/Tsiory Andriantsoarana

Udongo mweupe na rojo la ukwaju ndio mlo wa wengi kusini mwa Madagascar

Miaka mitatu mfululizo ya ukame kusini mwa Madagascar, imekuwa mwiba kwa wakazi wa eneo hilo kwa kuwa mazao yamekauka na ongezeko la vimbunga vya mchanga kwenye ardhi yenye rutuba, limesababisha wakulima washindwe kupanda mazao na sasa wanakabiliwa siyo tu na njaa bali pia utapiamlo uliokithiri. Assumpta Massoi na maelezo zaidi. 

Taswira halisi ya njaa! Watoto wenye utapiamlo kwenye wilaya ya Amboasary, miongoni mwa watu 1,350,000 wanaokadiriwa kuwa na uhaba wa chakula katika wilaya 10 zinazokumbwa na ukame kusini mwa Madagascar. 

Sauti
2'13"

Napenda somo la kemia, nataka kuwa daktari- Mwanafunzi Mkimbizi Sudan Kusini

amishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, Filippo Grandi akiwa ziarani barani Afrika, ametembelea wanafunzi katika shule inayofanya vizuri zaidi kimasomo kwa wakimbizi na wenyeji nchini humo na akaongeza wito wa uwekezaji zaidi katika elimu kwa watu waliofurushwa na pia jamii zinazowakaribisha. Taarifa ya Grace Kaneiya inaeleza zaidi. 

Sauti
1'50"
UN Photo/Mokhtar Mohamed

Wakimbizi wa ndani Somalia wahitaji msaada zaidi

Wakimbizi wa ndani nchini Somalia ni mtihani mkubwa ambao mratibu mkazi wa Umoja wa Mataifa na wa masuala ya kibinadamu nchini humo  Adam Abdelmoula, akiwa ziarani mjini  Baidoa amesema linahitaji dawa mujarabu na ya muda mrefu. Jason Nyakundi na taarifa kamili .

Mjini Baidoa baada ya kuwasili na kukutana na wenyeji wake  hasa kutoka Umoja wa Mataifa Bwana Abdelmoula alifunga safari hadi kwenye makazi ya maelfu ya wakimbizi wa ndani ya Hataatafor kusikiliza vilio vyao. 

Sauti
2'35"
UN

Watu wasafirishwa kiharamu ili kutumikishwa kwenye kuombaomba

Idadi ya watoto wanaosafirishwa kiharamu imeongezeka mara tatu katika kipindi cha miaka 15 iliyopita, huku idadi ya wavulana kwenye kundi hilo ikiwa imeongezeka mara 5, imesema ripoti mpya ya ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabili uhalifu na madawa ya kulevya, UNODC. Taarifa zaidi na Assumpta Massoi.

Ripoti hiyo ya usafirishaji haramu wa binadamu duniani yam waka 2020  imezinduliwa mjini Vienna, Austria ikifafanua zaidi kuwa watoto wa kike wanasafirishwa kiharamu kwa ajili ya kutumikishwa kingono ilihali wavulana kutumikishwa kwenye ajira.

Sauti
3'8"