Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

OCHA/Christian Cricboom

Burundi sasa ni shwari tuungeni mkono katika uchaguzi:Nibigira

Waziri wa mambo ya nje wa Burundi Ezechiel Nibigira ameiambia Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa kuwa anakusudia baadaye hii leo kuuleza mjadala mkuu wa mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA74 pamoja na mambo mengine, kuhusu hatua za maendeleo ambazo Burundi imepiga na pia kuiomba jumuiya ya kimataifa kuiunga mkono nchi yake.

Sauti
2'12"
UNnewskiswahili/Patrick Newman

Kucheza kamari sio uwekezaji- Kituyi

Katibu Mkuu wa kamati ya biashara na maendeleo ya Umoja wa Mataifa, UNCTAD Dkt. Mukhisa Kituyi amesema teknolojia ya kuwa na fedha kwenye mtandao wa simu hadi mashinani itakuwa na maana zaidi pale watu watatumia fedha hizo kujiongezea kipato. 

Sauti
3'11"
UN/Cia Pak

Elimu, ujumuishwaji na mabadiliko ya tabianchi ni baadhi vya vipaumbele vya Kenya aeleza Rais Uhuru Kenyatta

Tumefika hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa kuungana na nchi wanachama kuelezea ambayo Kenya imeyafanya katika kuhakikisha inaendana na vipaumbele vya mkutano huu wa Baraza Kuu la Umoja huo UNGA74 ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, ujumuishwaji na ushirikiano wa kuhakisha utimizaji wa malengo ya maendeleo endelevu SDGs ifikapo mwaka 2030.

Sauti
2'4"