Tuchukue hatua Mediteranea irejee katika hali yake ya awali- Guterres
Fursa za kiuchumi na kijamii kwenye ukanda wa Mediteranea ambao kihistoria unatambulika kwa maendeleo ya kitamaduni, hivi sasa ziko mashakani kutokana na ukanda huo kughubikwa na matatizo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema hayo akihutubia kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kilichokutana leo kujadili changamoto za amani na usalama kwenye ukanda huo unaojumuisha nchi zote zinazozingira bahari ya Mediteranea.