UNVIM yaanza kazi kurahisisha usafirishaji bidhaa Yemen
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amekaribisha uzinduzi rasmi wa utendaji wa chombo cha umoja huo cha kuthibitisha usafirishaji wa bidhaa za huduma na kibiashara nchini Yemen, UNVIM, kwa mujibu wa azimio la baraza la usalama namba 2216 la mwaka 2015.