Mauaji ya Burundi ni dhihirisho la machafuko yanayoenea- Zeid
Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu katika Umoja wa Mataifa, Zeid Ra’ad Al Hussein, amelaani idadi inayoongezeka ya mashambulizi dhidi ya maafisa waandamizi wa serikali nchini Burundi, kufuatia mauaji ya Brigedia-Jenerali Athanase Kararuza na mkewe, na jaribio la kumuua waziri siku moja kabla.