Kinga dhidi ya COVID-19 yaleta fursa ya kipato kwa mwanamke mjasiriamali, Uganda
Mlipuko wa virusi vya corona duniani umekwamisha uchumi wa mataifa mengi na vyanzo vya mapato kwa watu wa karibu tabaka zote. Hata hivyo wale ambao wameweza kupunguza athari za maradhi haya kiuchumi ni wajasiriamali wabunifu wanaobadilika na mazingira yaliyopo.