Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Mashariki ya Kati

Familia huko Gaza zinatatizika kupata chakula cha kutosha.
© WFP/Ali Jadallah

Baada ya kulazimishwa kuondoka Rafah baadhi ya wapalestina warejea kwenye nyumba zao zilizoathiriwa na mabomu

Kuongezeka kwa shughuli za kijeshi huko Rafah, kusini mwa Gaza, kumesababisha mamia kwa maelfu ya watu kuyahama makazi yao, na kufanya maisha kuwa magumu zaidi kwa maelfu ya familia ambazo tayari zimelazimika kuyahama makazi yao mara kadhaa. Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa chakula duniani WFP lina wasiwasi mkubwa kwamba hali hii ya kuhama hama inaweza kusababisha janga la kibinadamu, nakupelekea kusimama kwa shughuli za kutoa misaada ya kibinadamu.

Sauti
2'32"
Familia ya kipalestina ikiwa inaondoka eneo la Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza
© UNICEF/Eyad El Baba

UNRWA: Waliokimbia Rafah wafikia 800,000

Kwa mara nyingine tena karibu nusu ya wananchi wote waliokuwa Rafah au watu 800,000 hivi sasa wapo njiani wakilikimbia eneo hilo ambalo lilianza kushambuliwa na jeshi la Israel Mei 6 mwaka huu baada ya kutolewa kwa amri na jeshi la Israel la kuwataka watu wote kuondoka eneo hilo.