Vifijo na nderemo vyashamiri Bentiu wakati wa ziara ya mkuu wa UNICEF

Kufuatia uteuzi wake kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEF, Henrietta Fore amefanya ziara huko Sudan Kusini.
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF amehitimisha ziara yake huko Sudan Kusini ambako licha ya kushuhudia madhila yanayokumba watoto ikiwemo utapiamlo uliokithiri , ameleta faraja kwa familia zilizokuwa zimetengana na watoto watoto wao. Siraj Kalyango na taarifa zaidi.
(Taarifa ya Siraj Kalyango)
Nats..
Nchini Sudan Kusini, katika moja ya miradi ya maji ya mto Nile, Henriette H. Fore, Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEF akiwasili na kulakiwa kukagua mradi wa maji yanayotumiwa na wakimbizi wa ndani…
Nats..
Alielezwa na wauguzi jinsi wanavyokuwa na mtihani kwani watoto wagonjwa ni wengi lakini nafasi ya matibabu ni ndogo.
Nats..
Nats..
Wanawake katika kituo cha wakimbizi wa ndani cha Bentiu walishindwa kuficha furaha yao na kumbeba juu juu Bi. Fore!
Nats…