Sitisheni mapigano Syria tufikishe misaada- UN
Nchini Syria hakuna dalili zozote za mapigano kumalizika huku watoto walionasa kwenye mzozo huo wakiendelea kukumbwa na jinamizi kila uchao.
Hiyo ni kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF Henrietta H. Fore katika taarifa yake iliyotolewa New York, Marekani.
Amesema anavunjika moyo kwa kile ambacho watoto wa Syria wameendelea kukabiliana nacho kutokana na vitendo vya watu wazima, vitendo ambavyo amesema vinapuuza kabisa ulinzi, usalama na ustawi wa watoto.