Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Henriette H. Fore

UNICEF/Khuder Al-Issa

Sitisheni mapigano Syria tufikishe misaada- UN

Nchini Syria hakuna dalili zozote za mapigano kumalizika huku watoto walionasa kwenye mzozo huo wakiendelea kukumbwa na jinamizi kila uchao.

Hiyo ni kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF Henrietta H. Fore katika taarifa yake iliyotolewa New York, Marekani.

Amesema anavunjika moyo kwa kile ambacho watoto wa Syria wameendelea kukabiliana nacho kutokana na vitendo vya watu wazima, vitendo ambavyo amesema vinapuuza kabisa ulinzi, usalama na ustawi wa watoto.

Sauti
1'35"

Sudan Kusini ni hatari kwa watoa misaada-UNICEF

Hali ya sasa ya kiusalama nchini Sudan Kusini si shwari kwa wafanyakazi wanaotoa misaada.

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, Henrietta H. Fore amesema hayo leo akieleza kuwa shirika lake pamoja na mengine ya misaada nchini Sudan Kusini yanafanya kazi katika mazingira hatari wakati wakitoa misaada muhimu inayohitajika kwa watoto pamoja  na vijana.