Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sudan Kusini ni hatari kwa watoa misaada-UNICEF

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, Henrietta H. Fore asikiliza simulizi kutoka wafanyakazi wa UNICEF katika ziara yake nchini Sudan Kusini. Picha: UNICEF/UN0156591/Prinsloo

Sudan Kusini ni hatari kwa watoa misaada-UNICEF

Hali ya sasa ya kiusalama nchini Sudan Kusini si shwari kwa wafanyakazi wanaotoa misaada.

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, Henrietta H. Fore amesema hayo leo akieleza kuwa shirika lake pamoja na mengine ya misaada nchini Sudan Kusini yanafanya kazi katika mazingira hatari wakati wakitoa misaada muhimu inayohitajika kwa watoto pamoja  na vijana.

image
Wanaume wanakusanya maji kutoka kwa pampu inayotega maji kutoka mto Nile, moja ya programu ya maji mjini Juba. Picha:UNICEF/UN0156591/Prinsloo
Akizungumza baada ya ziara yake ya siku mbili siku mbili nchini humo ili kujionea hali ya utoaji misaada ilivyo kwa sasa, Bi. Fore amekariri kauli ya kuwa Sudan Kusini ndio taifa hatari zaidi kwa mashirika ya kutoa misaada.

Ameeleza kuwa mwaka uliopita pekee, wafanyakazi 28 wa kutoa misaada waliuawa, ilhali mashirika  hayo yanaendelea kutoka misaada kwa watoto walio katika shida.

image
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, Henrietta H. Fore asikiliza simulizi kutoka mama mmjoja nchini Sudan Kusini. Picha: UNICEF/UN0156591/Prinsloo
Wakati wa ziara hiyo alisikiliza simulizi za masahibu kutoka kwa waathirika wa mzozo huo akiwemo mwanamke ambae anasema alilazimika kutembea kwa siku kadhaa  akitafuta msaada wa mtoto wake aliyekondeana kutokana na utapiamlo.

Pia alizungumza na kijana  wa umri wa miaka kumi alielazimishwa kujiunga na kundi moja la wapiganaji.

Vile vile alipata wasaa kukutana na watoto wawili ndugu ambao walitenganishwa na wazazi wao wakati mapigano yalipolipuka Bentiu mwaka 2010.

image
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, Henrietta H. Fore(kati) laini ya pili akiwa na wafanyakazi waa UNICEF nchini Sudan Kusini. Picha: UNICEF/UN0156591/Prinsloo
Mwaka jana UNICEF na wadau walitoa chanjo kwa watoto karibu milioni tisa dhidi ya surua huku wengine  laki moja na elf nane dhidi ya utapia mlo na  kuwasaidia watoto laki tatu kupata elimu.