Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM wapongeza hatua ya kuruhusu ndege za misaada kuingia Yemeni

Waathirika wa mizozo yemen. Picha: UNHCR

UM wapongeza hatua ya kuruhusu ndege za misaada kuingia Yemeni

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharura OCHA limefurahishwa na  taarifa ya  ujumbe wake huko Riyad Falme za kiarabu kwamba ndege ya abiria ya shirika hilo UNHAS imeruhusiwa kuanza safari zake  kutoka Amman kwenda Sana’a nchini Yemen kuanzia kesho  Jumamosi.

Kwa mujibu wa Jens Laerke msemaji wa OCHA japo hawajapata ufafanuzi kuhusu kupata ruhusa za safari kutoka  bandari ya  Hudayday na Saleef kwajili ya kusafirisha mahitaji ya kibunadamu, amefurahishwa na zoezi hilo la awali  na kwamba  UM unategemea kupata ruhusa ya ndege zigine kutoka DJibouti kuelekea Sana’a.

(Sauti ya Jens Laerke )

“Kama Mashirika ya kibinadamu tunatoa misaada kwa watu milioni 7 Yemen ambao kimsingi wanatutegema kwa kila kitu. Kwa mfano tunasambaza maji kwa takribani watu milioni 4 wakati huu wa jaa kali nchini  humo.”

Aidha Jens amesema zoezi la kupeleka misaada pia litasaidia kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu ambao umekua tishio kwa watu wengi nchini Yemeni kutokana na kukosa huduma ya maji safi.