Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Machozi na furaha watoto wakikutanishwa na wazazi wao nchini Sudan Kusini

Machozi na furaha watoto wakikutanishwa na wazazi wao nchini Sudan Kusini

Kulingana na takwimu za Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, takriban watoto 4,000 wamekutanishwa na wazazi wao tangu vita na vurugu uzuke nchini Sudan Kusini mwaka 2013. Kambi la wakimbizi wa ndani, Bor, lilitengwa kwa ajili ya watoto waliotenganishwa na wazazi wao, lengo kubwa likiwa ni kuwawezesha watoto hao kuenda shule.

Katika makala hii, tunakutana na mtoto wa kike Nyanaeda ambaye ni mmoja wa watoto wakimbizi nchini humo waliokutanishwa na wazazi. Ungana na Flora Nducha kwa undani zaidi...