Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Muarubaini wa suluhu ya Burundi ni makubaliano ya Arusha: Balozi Manongi

Muarubaini wa suluhu ya Burundi ni makubaliano ya Arusha: Balozi Manongi

Suluhu la mgogoro wa kisiasa nchini Burundi lazima litokane na misingi ya makubaliano  ya Arusha  ambayo ilizaa matumaini kwa taifa hilo la Afrika Mashariki,  amesema mwakilishi wa kudumu wa Tanzania katika ofisi ya Umoja wa Mataifa mjini New York Balozi Tuvako Manongi.

Katika mahojiano na Joseph Msami wa idhaa hii muda mfupi baada ya kulihutubia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa, Balozi Manongi anaanza kuelezea ujumbe aliouwasilisha kwenye baraza hilo lililojadili hali ya amani na usalama nchini Burundi.