Machafuko yakiendelea Sudan na Sudani Kusini vikwazo viwekwe: Dk Salim
Wakati baraza la usalama la Umoja wa Mataifa likikutana leo kwa mashauriano kuhusu hali nchini Sudan na Sudan Kusini mwanadiplomasia na mmoja wa wapatanishi wa mgogoro nchini humo kupitia muunganao wa Afrika AU Dk Salim Ahmed Salim, amesema pamoja na juhudi za upatanishi bado machafuko yanaendelea na kuwaumiza wananchi wasio na hatia.
Katika mahojiano maalum na idhaa hii Dk Salim amesema ikiwa upatanishi wa mazungumzo ukishindikana uwekwaji wa vikwazo utumike
(SAUTI DK SALIM)