Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.
Taarifa kuhusu Virusi vya Corona
COVID-19: Maandalizi ya kuelekea “kawaida mpya” katika makao makuu ya UN
"Usalama na afya ya wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa, wawakilishi wa nchi wanachama na wale wote ambao wanatumia jengo letu, ni kipaumbele cha kwanza. Kurejea kwa wafanyakazi jengoni kutazingatia mapendekezo ya jiji na jimbo la New York, ambayo watafuata kadri yatakavyokuja.” Atul Khare, Msaidizi wa Katibu Mkuu katika Operesheni.
Wagonjwa wasio na dalili kali za COVID-19 Kenya kutibiwa nyumbani
Idadi ya wagonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 nchini Kenya ikifikia 300, serikali hii leo imetangaza mkakati wa kuepusha vituo vya afya na hospitali kuzidiwa uwezo wa kutibu wagonjwa hao.
Msemaji wa serikali ya Kenya Cyrus Oguna akizungumza jijini Nairobi, Kenya, amesema kuwa wagonjwa waliothibitishwa kuwa na virusi watatibiwa hospitalini, lakini wale wasio na dalili zozote za ugonjwa wataugulia makwao.
10 JUNE 2020
Tenki za maji Mathare, Nairobi ni lulu katikati ya janga la COVID-19
Maambukizi mapya ya ugonjwa wa virusi vya Corona au COVID-19, yakiendelea kuripotiwa nchini Kenya, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF nchini humo limeanzisha zaidi ya vituo 1000 vya kunawa mikono katika eneo la makazi duni la Mathare kwenye mji mkuu Nairobi, kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi mapya.
Wagonjwa wasio na dalili kali za COVID-19 Kenya kutibiwa nyumbani
Idadi ya wagonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 nchini Kenya ikifikia 3000, serikali hii leo imetangaza mkakati wa kuepusha vituo vya afya na hospitali kuzidiwa uwezo wa kutibu wagonjwa hao.