Wagonjwa wasio na dalili kali za COVID-19 Kenya kutibiwa nyumbani
Idadi ya wagonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19 nchini Kenya ikifikia 300, serikali hii leo imetangaza mkakati wa kuepusha vituo vya afya na hospitali kuzidiwa uwezo wa kutibu wagonjwa hao.
Msemaji wa serikali ya Kenya Cyrus Oguna akizungumza jijini Nairobi, Kenya, amesema kuwa wagonjwa waliothibitishwa kuwa na virusi watatibiwa hospitalini, lakini wale wasio na dalili zozote za ugonjwa wataugulia makwao.
Ukurasa kuhusu virusivyacorona & taarifa mpya
Wasomaji wanaweza kupata taarifa na muongozo kuhusu mlipuko wa virusi vya corona (2019-nCoV) kutoka Umoja wa Mataifa, Shirika la afya duniani na mashirika mengine ya UN hapa. Kwa habari mpya kila siku kutoka UN News, bofya hapa.Idadi ya wagonjwa wa COVID-19 imeongezeka kwa kasi tangu mgonjwa wa kwanza aripotiwe mwezi Machine mwaka huu na idadi ya wagonjwa inatarajiwa kuongezeka kutokana na kuendelea kwa upimaji wa virusi hivyo.
Akizungumzia hatua ya leo ya serikali, Dkt. Ahmed Khalebi kutoka maabara ya Lancet anasema kuwa hatua ya kuwatibia wagonjwa majumbani ingeanza kitambo