Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Taarifa kuhusu Virusi vya Corona

Virusi vya Corona kama dharura ya afya ya umma:Taarifa za UN News Kiswahili
Mlipuko uliripotiwa mara ya kwanza Wuhan China Desemba 31, 2019

Ukurasa huu unaleta pamoja taarifa kuhusu muongozo kutoka kwa Shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO na Umoja wa Mataifa kuhusu mlipuko wa sasa wa virusi vya corona au COVID-19, ambavyo viliripotiwa mara ya kwanza Wuhan, China mnamo Desemba 31, 2019. Tafadhali tembelea ukurasa huu kupata taarifa za kila siku. WHO inafanya kazi kwa karibu na wataalam wa kimataifa, serikali na wadau kupanua ujuzi wa kisayansi kuhusu virusi hivi vipya, kutokana na jinsi vinavyosambaa na athari zake  na kutoa ushauri kwa nchi na watu, kuhusu hatua za kuchukua kwa ajili ya kulinda afya na kuzuia kuenea kwa mlipuko.

© UNICEF/Lisa Adelson

Uwepo wa COVID-19 unazua hatari kwa watoto muda waliopo mtandaoni

Mamilioni ya watoto wako hatarini kudhurika wakati huu ambao maisha yao yamehamia zaidi mitandaoni wakati wa kukaa ndani kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19, imeeleza taarifa iliyotolewa hii leo mjini New York Marekani na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF pamoja na wadau wake. Jason Nyakundi na maelezo zaidi
 
(Taarifa ya Jason Nyakundi)
 

Sauti
2'55"
UN Photo/Evan Schneider

Si wakati wa kupunguza rasilimali kwa shirika lolote lile la kibinadamu linalopambana na COVID-19-Guterres

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema huu si wakati wa kupunguza rasilimali za kufanikisha operesheni za shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO. Grace Kaneiya na ripoti kamili.
 
(Taarifa ya Grace Kaneiya)
 
Bwana Guterres amesema hayo katika taarifa iliyotolewa Jumanne usiku na msemaji wake jijini New York, Marekani akisema kuwa siyo tu kwa WHO bali pia si wakati wa kupunguza rasilimali kwa shirika lolote lile la kibinadamu linalopambana hivi sasa na ugonjwa wa virusi vya Corona, COVID-19.
 

Sauti
2'2"