Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis (kushoto) akiwa na Rais wa DRC  Felix-Antoine Tshisekedi jijini Kinshasa tarehe 31 Januari 2023
Ofisi ya Rais

DRC: Papa Francis ataka silaha ziwekwe chini, na wanaopora mali waondoke

Kiongozi wa kanisa katoliki duniani, Papa Francis aliyeko ziarani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC amewasihi wakristo waweke silaha chini na badala yake wakumbatie huruma ya Mungu nchini humo. Radio Okapi ya Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO imesema Papa Francis amesema hayo leo  wakati akihubiri kwenye misa iliyofanyika leo kwenye eneo la Ndolo, kitongoji cha Barumbu kwenye mji mkuu wa DRC, Kinshasa. 

Watu walioyakimbia makazi yao katika eneo la Equatoria Magharibi Sudan Kusini wakikutana na viongozi wa vijiji.
UNMISS

Maelfu ya wakimbizi wa ndani wa Tambura warejea makwao

Sudan Kusini ni moja ya nchi iliyoathirika kwa muda mrefu na vita vya wenyewe kwa wenyewe ambapo mara kwa mara makundi ya wapiganaji wenye silaha yalikuwa yakivamia katika vijiji na kuwaua raia na kupora mali zao. Kutokana na sababu hiyo wananchi wengi wamekuwa wakikimbilia katika kambi za kijeshi zilizoko karibu na maeneo yao ili kusaka hifadhi.

Sauti
4'9"
Kikosi cha kulinda amani cha Tanzania nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati CAR wakizungumza na kamanda wa kikosi.
Photo: MINUSCA/Honorine Guehi Niare Yao

Viongozi wa Mambéré-Kadéï wawashukuru TANBAT 6 kwa kutambua ushirikiano

Viongozi wa eneo la utawala la Mambéré-Kadéï nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR wamewashukuru viongozi wa walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania wanaohudumu chini ya ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MINUSCA katika eneo hilo la Berbérati kwa kutambua kuwa ulinzi wa amani unategemea ushirikiano wa wageni na wenyeji.

Sauti
1'55"