Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Sedelia Abdullahi ni mhudumu wa afya wa mstari wa mbele huko mashinani nchini Ethiopia na kila siku huchunguza na kutibu watoto wenye utapiamlo kwenye kituo cha afya cha kambi ya wakimbizi ya Bambassi nchini Ethiopia kilichojengwa na UNICEF kwa ufadhili …
UNICEF Ethiopia

Wahudumu wa afya Ethiopia warejesha tabasamu kwa watoto- UNICEF

Nchini Ethiopia, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto duniain, UNICEF kupitia msaada kutoka Muungano wa Ulaya umewezesha mamia ya wahudumu wa afya walio mstari wa mbele kila uchao kuweza kutembelea wakimbizi wa ndani waliofurushwa makwao kutokana na mzozo kwenye jimbo la Benishangul-Gumuz lililoko kaskazini-magharibi mwa taifa hilo, likipakana na Sudan ili kuwapatia huduma za lishe bora wakati huu ambapo watoto wanakabiliwa na utapiamlo.

Sauti
2'31"