Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kambi ya wakimbizi ya Za'atari nchini Jordan inayoonekana kutoka juu ina wakimbizi kutoka Syria.
UN Photo/Mark Garten)

Watoto wangu wananiuliza Syria ni nini? Kambi ya Zaatar ikiingia muongo mwingine

Mwaka 2022 ni  miaka 10 tangu kuanzishwa kwa kambi ya wakimbizi ya Za’atari nchini Jordan, kambi ambayo inasimamiwa na Umoja wa Mataifa. Ni kambi kubwa zaidi Mashariki ya Kati na moja ya kambi kubwa zaidi duniani ikiwa ni maskani ya wasyria 80,000. UN News au Habari za UN imezungumza na baadhi ya wakimbizi kuhusu maisha katika kambi hiyo, na matumaini yao kwa siku zijazo. 

Waathirika wa mafuriko kwenye eneo la Balochistan, nchini Pakistani.
WFP Pakistan

Msifurishe dunia hii leo, wala msiizamishe kesho- Ujumbe wa Katibu Mkuu wa viongozi wa dunia

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amezungumza na waandishi wa habari jijini New York, Marekani hii leo ikiwa ni kuelekea Mjadala Mkuu wa Baraza Kuu la UN unaoanza wiki ijayo akisema ujumbe wake mkuu kwa viongozi watakaoshiriki ni dhahiri ya kwamba wachukue hatua kupunguza kiwango cha joto duniani.

Sauti
3'45"
Sidonie, mwenye umri wa miaka 10, akiwa mbele ya darasa la shule yake ya msingi Kitambo iliyoko mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, Kinshasa.
© UNICEF/Josue Mulala

Elimu ya sasa inapitia janga kubwa: Tuirekebishe kwa mustakabali wa watoto

Ingawa msemo wa haki ya binadamu umezoelekea, hakuna haki ya binadamu yoyote ambayo imetolewa bure bila kupiganiwa, vivyo hivyo inapaswa kuwa kwa elimu, amesema Leonardo Garnier, Mshauri Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mkutano wa Ngazi ya juu wa Umoja wa Mataifa kuhusu marekebisho ya mfumo wa elimu duniani, mkutano unaoanza Ijumaa hii kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa. Kufahamu msingi wa kauli hiyo, 

Sauti
2'
Tarehe 16 mwezi Juni mwaka 2022 mtoto wa kike akitumia pampu ya mkono kupata maji kutoka bwawa la mchanga lililojengwa na UNICEF huko Kanyangapus kaunti ya Tukrana nchini Kenya.
© UNICEF/Paul Kidero

Mabwawa ya mchanga Turkana yaepusha wanawake kutembea kilometa 10 kusaka maji

Katika Kijiji cha Kanyangapus Kaunti ya Turkana nchini Kenya hali ya ukame ni mbaya sana kila kona na moja ya athari kubwa zilizoambatana nao ni ukosefu wa maji.  Mabwawa ya mchanga yamekuwa suluhu bunifu inayozisaidia kaunti nyingi zilizo katika hali ya nusu jangwa nchini Kenya na shukrani kwa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF kwa kufadhili wa mradi huo wa ujenzi wa mabwawa ya mchanga na pampu za maji, sasa adha ya maji katika kaunti ya Turkana imepungua na hususan kwa wanawake wanaolazimika kwenda umbali mrefu kusaka maji. 

Sauti
2'40"