Vita, Machafuko na majanga mengine vyatawanya watoto milioni 36.5 mwaka 2021: UNICEF
Vita, machafuko na mjanga mengine vimewaacha watoto milioni 36.5 wakitawanywa kutoka majumbani kwao hadi kufikia mwisho wa mwaka 2021 kwa mujibu wa takwimu mpya zilizotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF ambalo linasema idadi hiyo ni kubwa kabisa kurekodiwa tangu vita ya pili ya dunia.