Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akizungumza na waandishi wa habari pamoja na Rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine
UN /Eskinder Debebe

Guterres awaambia waukraine 'dunia inawaona' huku akiahidi msaada zaidi

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameielezea Ukraine kama "kitovu cha maumivu na zahma isiyovumilika", alipozungumza na wanahabari leo mjini Kyiv akiwa pamoja na mwenyeji wake rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine na kuahidi kuongeza msaada kwa watu wa taifa hilo huku kukiwa na mateso makubwa , na mamilioni ya watu wamekimbia makazi yao kutokana na uvamizi wa Urusi. 

Nataliia Vladimirova na binti yake Oleksandra au Sasha kwenye umri wa miaka 4 wakiwa mjini Lisbon ,Ureno ambako waliwasili tarehe 14 Machi 2022 wakikimbia vita nchini mwao Ukraine
UN News/Leda Letra.

Ukraine: Hofu yangu ni mume wangu- Nataliia

Nataliia Vladimirova alikimbia nyumbani kwake Kharkiv, Ukraine, siku ya kwanza tu Urusi  ilipovamia nchi yao tarehe 24 mwezi Februari, 2022, akiambatana na binti yake Oleksandra mwenye umri wa miaka 4 pamoja na mama mkwe wake. Wao ni miongoni mwa maelfu ya wakimbizi wa Ukraine waliopata hifadhi ya muda nchini Ureno . Akihojiwa na Idhaa ya Umoja wa Mataifa huko Ureno, Nataliia al maaruf Natasha, anasimulia simulizi wa yale aliyopitia ikiwemo kugawanyika kwa familia sambamba na kupoteza wengine.