Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Serikali ya Somalia kuanza mazungumzo ya amani mjini Khartoum

Wajumbe wa serekali ya mpito ya Somalia na wale wa Baraza la mahakama ya kiislamu linalodhibiti mji mkuu wa Mogadishu na sehemu kubwa ya nchi, wanaanza duru ya pili ya mazungumzo ya amani mjini Khartoum hii leo. Abdushakur Aboud amezungumza na mbunge na waziri mdogo wa zamani Hussein Bantu huko Baido na kumuliza kwanza mazungumzo yatahusu masuala gani. ~~

Njia za kudumisha amani na maendeleo nchini Somalia

Mjumbe maalum wa Katibu mkuu huko Somalia Bw Francois Fall alikutana na kundi la wajumbe wa kimataifa linalo jaribu kutafuta njia za kudumisha amani na maendeleo katika taifa hilo la pembe mwa afrika na kujadili njia za kuimarisha msaada wa kimataifa katika juhudi zao

Wagombea urais nchini DRC wakubali kuunda tume

Afisi ya Umoja wa mataifa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, MONUC ilitangaza wiki hii kuwa wagombea wawili walobaki wa kiti cha rais huko kutokana na uchaguzi wa mwezi uliyopita, wamekubaliana kuunda tume ya pamoja kuchunguza ghasia zilizotokea baada ya kutolewa matokeo ya awali,