Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Mtoto mwenye umri wa mwaka 1 anafanyiwa unchunguzi wa matibabu kama kuna dalili za utapiamlo katika kituo cha mapokezi kwenye mpaka wa Sudan na Sudan Kusini.
© WFP/Hugh Rutherford

Uongozi wa jimbo la Upper Nile nchini Sudan Kusini waomba usaidizi zaidi wa ulinzi

Huku mzozo wa Sudan ukiendelea, wakimbizi na wanaorejea wanamiminika katika mipaka ya nchi jirani ya Sudan Kusini, wengi wamekuwa wakitafuta hifadhi katika jimbo la Upper Nile nchini humo na wanahitaji msaada wa haraka wa kibinadamu.  Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Kusini UNMISS umefanya mazungumzo na uongozi wa jimbo hilo kuona namna ya kuwasaidia.

Sauti
2'25"
Dennis Francis, Rais wa kikao cha 78 cha Baraza Kuu, akitoa muhtasari wa vipaumbele vyake kwa 2024. (Maktaba)
UN Photo/Eskinder Debebe

Rais wa Baraza Kuu: Umoja wa Mataifa sio tatizo

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Dennis Francis Pamoja na mambo mengine amesema Umoja wa Mataifa "sio tatizo" bali tatizo linatokana na kwamba baadhi ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa wanahisi wanaweza kukiuka mkataba wa Umoja wa Mataifa watakavyo na kukiuka sheria za kimataifa bila kuadhibiwa.

UNFPA na wadau waendelea kutoa baadhi ya huduma za kuokoa maisha kwa wanawake wajawazito
© PMRS Gaza

Gaza: Huku wanakimbia vita wanawake wa Gaza inakuwaje wakiwa katika hedhi?

Kunapozuka mizozo na machafuko wananchi wote wanaathirika kwasababu maisha yao yanaparanganyika kabisa tofauti na walivyokuwa wamezoea. Watoto waliokuwa wakienda shule sasa hawaendi, si wafanyabiashara, wakulima wala viongozi wa dini wanaotekeleza majukumu yao ya kila siku na suala moja lililo kweli kwa kila mtu ni kuwa wanatafuta kila namna ya kuokoa maisha yao na wengi njia hiyo huwa ni kukusanya virango vyao kidogo wanavyoweza kubeba na kukimbia kuokoa nafsi zao. 

Uvutaji wa tumbaku unaunaathiri afya yako.
© Unsplash/Andres Siimon

Nilivuta sigara tangu mtoto, acheni haina maana- Thierry

Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, simulizi ya mtu aliyeanza kuvuta sigara akiwa kijana balehe na sasa ameamua kuacha inamulika ni kwa nini shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani, WHO linasisitiza umuhimu wa kampeni za kuacha tumbaku kwani ni miongoni mwa visababishi vikubwa vya maambukizi ya saratani ya mapafu inayooongoza kwa kuua zaidi vifo miongoni mwa wanaume duniani. 

Sauti
2'26"