Umoja wa Mataifa na wadau wazindua kampeni ya #LetMeLearn kabla ya mkutano mkuu wa elimu
Janga la elimu likichangiwa na janga la COVID-19, Umoja wa Mataifa unashirikiana na shirika la kutoa misaada kwa watoto la Theirworld na wadau wengine katika sekta hiyo, kuzindua kampeni ya #LetMeLearn au ‘Hebu nijifunze’, na kuwataka viongozi wa dunia kusikiliza sauti za vijana na kuweka mipango na fedha zinazohitajika ili kutoa elimu bora kwa kila mtoto.