Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari Mpya

Malori yaliyosheheni msaada wa kibinadamu yakijiandaa kuingia Gaza kupitia kivuko cha Rafah
© UNICEF/Eyad El Baba

Mashirika ya UN yaomba kufunguliwe njia nyingine ya kufikisha misaada Gaza

Zikiwa ni zaidi ya siku 100 tangu kuibuka upya kwa mzozo huko Mashariki ya Kati, mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo yametoa taarifa inayoelezea kuongezeka kwa hatari ya baa la njaa na milipuko ya magonjwa ya kuambukiza huku yakisisitiza muarobaini pekee kwa sasa ni kuruhusu njia mpya za kuingiza misaada ya kwenda kutatua changamoto zinazowakabili wananchi walioko Gaza. 

Sauti
3'34"
Watu waliojeruhiwa wakisubiri kutibiwa katika hospitali ya Al Shifa mjini Gaza. (Maktaba)
© WHO

Mzozo Gaza: Hospitali zazidi kuzidiwa uwezo, wagonjwa sakafuni

Ikiwa leo ni siku ya 93 tangu mapigano yaanze huko Ukanda wa Gaza kati ya jeshi la Israel na wanamgambo wa kipalestina waliojihami, likiwemo kundi la Hamas, mashirika ya Umoja wa Mataifa ya usaidizi wa kiutu yanazungumzia uwepo wa idadi kubwa ya vifo miongoni mwa wanawake na watoto huku yakisihi timu za madaktari ziruhusiwe kuingia eneo la Gaza ili ziendelee na jukumu la kuokoa maisha. 

Sauti
2'16"
Lilly Kiden akibeba mazao ya mbogamboga kutoka kwa shamba lake.
FAO

Asante FAO kunijengea mnepo sasa najikimu mimi na familia yangu: Lilly Kiden

Wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP28 ukijiandaa kufunga pazia hapo kesho nakupeleka Sudan Kusini jimbo la Equatorial Mashariki ambako wakulima walioathirika na mabadiliko ya tabianchi sasa wanajengewa mnepo na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na wengi wameweza kujikwamua pamoja na familia zao. Ungana na Flora Nducha akikuletea safari ya mafanikio ya mmoja wa wanuafa wa mradi huo wa FAO. 

Sauti
2'8"
Kiwanda cha uzalishaji wa nishati ya jua kata kisiwa cha Unguja nchini Tanzania.
World Bank

Benki ya Dunia yasaidia ukuzaji wa rasilimali watu na maendeleo nchini Tanzania

Tarehe 19 Desemba mwaka 2019, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha azimio namba 74/245, ambalo liliteua tarehe 4 Desemba kuwa Siku ya Kimataifa ya Benki kwa kutambua mchango mkubwa wa benki za maendeleo za kimataifa na benki nyingine za maendeleo za kimataifa katika kuleta maendeleo endelevu na kuchangia uboreshaji wa hali za maisha za wananchi. 

Sauti
2'5"