Uganda yajihadhari kabla ya shari kwa kuchanja wahudumu wa afya dhidi ya Ebola:WHO
Kufuatia mlipuko wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC, mara mbili tangu mei mwaka huu, shirika la afya duniani WHO kwa kushirikiana na serikali ya Uganda wameanza kuchukua hatua ya kuwachanja wahudumu wa afya kuepusha kusambaa kwa ugonjwa huo ambapo tayari watu 180 wamethibitishwa kufariki dunia kutokana na Ebola.