Walinda amani wanajitoa kimasomaso- Guterres
Ulinzi wa amani unakumbwa na changamoto kila uchao ambapo walinda amani wanashambuliwa na kuuawa, lakini bado hawakati tamaa kwani lengo kuu ni amani na usalama duniani.
Ulinzi wa amani unakumbwa na changamoto kila uchao ambapo walinda amani wanashambuliwa na kuuawa, lakini bado hawakati tamaa kwani lengo kuu ni amani na usalama duniani.
Mizozo na njaa kali vyaendelea kuambatana kwenye maeneo kadhaa duniani na kuacha watoto, wanawake, wanaume, vijana kwa wazee hoi bin taaban. Baraza la Usalama lakumbushwa wajibu wake.
Bila msaada wa kibinadamu maisha ya raia wengi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) yako mashakani. Onyo hilo limetolewa na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anaehusika na masuala ya kuratibu misaada ya kibinadamu , Mark Lowcock wakati akilihutubia baraza la usalama la Umoja wa Mataifa hii leo na kuelezea hali ilivyo DRC.
Mfalme Iguru wa Pili, wa Bunyoro Kitara nchini Uganda anasifika sana kwa kitendo chake cha kila wakati kutumia hotuba zake kuhamasisha watu wake kujikinga dhidi ya UKIMWI na hii imezaa matunda hadi kupatiwa pongezi na Umoja wa Mataifa.
Hali ya usalama si shwari huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambapo mapigano baina ya makabila bila kusahau operesheni za kijeshi dhidi ya vikundi vilivyojihami vimesababisha maelfu ya watu kukimbilia nchi jirani. Uchaguzi unakaribia huku muda wa MONUSCO ukitarajiwa kuongezwa.
Kutoka Uganda shirika la Umoja wa Matifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR linasema mmiminiko wa wakimbizi kutoka nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasai ya Kongo (DRC), siku hizi umekuwa kinyume kabisa na matarajio , mwaka huu wakimbizi 60,000 wameingia, na kuibua changamoto katika utoaji wa misaada ya kibinadamu kwao.
Haki za binadamu zinazidi kusiginwa maeneo mbalimbali duniani hata katika nchi ambazo kwa muda mrefu zimetambuliwa kuwa visiwa vya amani, asema Zeid Ra'ad Al Hussein hii leo katika ripoti yake kuhusu hali ya haki za binadadamu duniani.