Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mabadiliko ya Tabianchi

Mabadiliko ya Tabianchi
Ujumbe kutoka kwa Katibu Mkuu

Lengo namba 13 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs linataka uhifadhi wa mazingira kwa kuchukua hatua muafaka. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio  Guterres akiwa ziarani katika nchi zilizoko ukanda wa pasifiki anapaza sauti ya kile kinachopaswa kufanywa kwa ubia ili kulinda sayari dunia kwa faida ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

UN News

COVID-19 imeongeza chumvi katika kidonda changu cha athari za mabadiliko ya tabianchi-Jemima Hosea 

Kutokana na mwamko wa watu nchini Tanzania kuyapenda mazingira ya nyumba zao, Jemima Hosea wa jijini Dar es Salaam, aliona hiyo ni fursa ya yeye kujipatia kipato kwa kuotesha na kuuza maua ya aina mbalimbali. Katika kipindi ambacho biashara yake ilikuwa imeanza kushamiri ndipo likaibuka janga la virusi vya corona vinavyosababisha ugonjwa wa COVID-19. Janga hili likaongeza machungu katika changamoto aliyokuwa anapambana nayo mfanyabiashara huyu-changamoto ya mabadiliko ya tabianchi. Stella Vuzo wa Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa amemtembelea Jemima na kutuandalia makala hii. 

Sauti
2'49"