15 Julai 2019
Pakua
Miongoni mwa yale anayokuletea assumpta Massoi katika Jarida letu la Habari leo ni pamoja na
-Kisa kipya cha Ebola chaibuka Goma DRC , shirika la afya WHO na serikali wanafanya kila njia kuzuia kusambaa kwa mlipuko huo
- Watoto milioni 20 hawakupata chanjo muhimu ya kuokoa maisha 2018 yasema mashirika ya UNICEF na WHO na kutaka kila nchi kuchukua hatua kuhakikisha watoto wote wanachanjwa
-Onyo limetolewa na shirika la afya duniani WHO kuwa vyakula vya watoto wachanga wa chini ya umri wa miezi sita vimejaa sukari
-Makala yetu leo inamulika uhifadhi wa mazingira ya bahari visiwani Zanzibar
-Na mashinani tuko Canada kwake Zipporah Ogot akiwaasa hususani wasichana kwamba elimu haichagui umri na haina kuchelewa
Audio Credit
UN News/assumpta Massoi
Audio Duration
12'15"