Maambukizi ya Ebola yapungua Kasai, DRC – WHO
Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO limesema mlipuko wa ugonjwa wa Ebola kwenye jimbo la Kasai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) bado upo lakini maambukizi yanapungua.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya duniani, WHO limesema mlipuko wa ugonjwa wa Ebola kwenye jimbo la Kasai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, (DRC) bado upo lakini maambukizi yanapungua.
Dozi karibu 45,000 za chanjo ya Ebola ziko njiani kuelekea jimboni Kasai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC huku Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF, likiongeza juhudi zake pamoja na serikali na wadau wake kulinda watoto na familia dhidi ya mlipuko wa hivi karibuni wa ugonjwa wa Ebola.
Chanjo dhidi ya virusi vya Ebola imeanza kutolewa hii leo kwa wahudumu wa afya pamoja na watu waliokuwa karibu na watu waliothibitishwa kuwa na ugonjwa wa Ebola katika eneo la Bulape ambalo ni kitovu cha ugonjwa huo huko jimboni Kasai nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Congo DRC, limesema leo shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO.
-Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nducha anakuletea UNGA79yafikia tamati hii leo na kupisha UNGA80 chini ya uongozi wa Rais mpya Annalena Baerbock
-Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyozinduliwa leo imesema matumizi ya kijeshi duniani yalifikia dola trilioni 2.7 mwaka 2024, yakiwa yameongezeka kwa zaidi ya asilimia 9 kutoka mwaka 2023
Mamlaka za afya nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC zimethibitisha mlipuko mpya wa ugonjwa wa Ebola katika Mkoa wa Kasai, huu ukiwa ni mlipuko wa 16 tangu virusi hivyo vilipotambulika kwa mara ya kwanza mwaka 1976 limesema leo Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani WHO
Uganda leo imetangaza rasmi mwisho wa mlipuko wa hivi karibuni wa homa ya Ebola, ikiwa ni chini ya miezi mitatu baada ya virusi hivyo kuthibitishwa katika mji mkuu Kampala limesema Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO
Mchango huu wa dola milioni 2 za Marekani kutoka kwa seriikali ya Sweden utatumika kwa muda wa miezi mitano kusaidia vipaumbele vya dharura vya mpango wa kitaifa wa Serikali ya Uganda wa kukabiliana na Ebola inayofahamika kama Ebola Sudan (EVD), kwa msisitizo maalum katika jiji la Kampala na sehemu zake tano za kiutawala, pamoja na wilaya za Mbale na Jinja.
Hii leo jaridani tunaangazia hali ya kibinadamu nchini Somalia na huduma zaa faya kwa wakimbizi wajawazito nchini Chad. Makala inatupeleka nchini Kenya na mashinani nchini Uganda, kulikoni?
Katika kudhihirisha ushirikiano wa kimataifa usio na kifani na hatua za haraka, wizara ya afya ya Uganda, Shirika la Afya la Umoja wa Mataifa Duniani WHO, na washirika wa kimataifa leo wamezindua jaribio la kwanza la kliniki la chanjo inayolenga aina ya virusi vyaebola vya Sudan.
Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya Afrika limetangaza rasmi kumalizika kwa ugonjwa wa Marburg nchini Equatorial Guinea baada ya kutogundulika uwepo wa mgonjwa yeyote kwa muda wa siku 42 tangu mgonjwa wa mwisho kuruhusiwa kutoka hospitalini.