Hakuna tena ugonjwa wa Marburg nchini Equatorial Guinea: WHO
Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni WHO kanda ya Afrika limetangaza rasmi kumalizika kwa ugonjwa wa Marburg nchini Equatorial Guinea baada ya kutogundulika uwepo wa mgonjwa yeyote kwa muda wa siku 42 tangu mgonjwa wa mwisho kuruhusiwa kutoka hospitalini.