Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Ebola

11 JANUARI 2023

Jaridan hii leo tutakupeleka nchini Uganda na Somalia. Makala tutamulika uanzishaji wa vikundi vya vijiji vya kukopa na kuweka akiba na kuimarisha ujuzi wa kidigitali na kifedha, na mashinani nchini tunakwenda nchini Ghana, kulikoni?

Sauti
12'35"
Uchunguzi wa virusi vya Ebola kwenye mpaka kati ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo , DRC na Uganda
WHO/Matt Taylor

Uganda yatangaza kutokomezwa kwa mlipuko wa Ebola

Uganda hii leo imetangaza kutokomeza mlipuko wa ugonjwa wa Ebola uliosababishwa na virusi aina ya Sudan, ikiwa ni chini ya miezi minne tangu kuthibitishwa kwa mgonjwa wa kwanza kwenye wilaya ya Mubende nchini humo 20 mwezi Septemba mwaka jana. Taarifa ya Thelma Mwadzaya inafafanua zaidi. 

 

Sauti
2'27"
Muuguzi akimtakasa mikono mgeni aliyetembelea hospitali ya mjini Masaka, Uganda
© UNICEF/Kalungi Kab

COVID-19 kuendelea kuwa mjadala 2023- WHO

Shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO limesema ingawa idadi ya vifo kutokana na ugonjwa wa COVID-19 ilipungua kwa mwaka jana wa 2022, bado tishio kutokana na ugonjwa huo linaendelea kwa mwaka huu wa 2023 na ugonjwa huo utaendelea kuwa mjadala na hatua zaidi za kinga na kitabibu zinapaswa kuendelea kuchukuliwa.

Paulina Ajello mfanyakazi wa WHO kitengo cha mawasiliano na ushirikishaji jamii akizungumza na wanajamii waelimishaji kuhusu Ebola.
Picha: WHO_Uganda/PhilipKairu

Jiji la Kampala laendesha kampeni ya kupambana na ugonjwa wa Ebola

Wakati huu ambapo hakuna mgonjwa mpya wa Ebola aliyesajiliwa katika mji mkuu wa Uganda tangu tarehe 14 Novemba, 2022 mamlaka ya afya ya Mji Mkuu wa Kampala kwa kushirikiana na Wizara ya Afya ya nchi hiyo hivi karibuni ilifanya kampeni ya siku saba kuelimisha umma ili kudumisha umakini wa watu na hatimaye kusaidia kumaliza mlipuko wa ugonjwa huo hatari duniani.

Natanael Melchor/Unsplash

Mwaka 2022 umegubikwa na changamoto lukuki za kiafya na kuweka rehani afya za mamilioni ya watu duniani: WHO

Shirika la afya la Umoja wa Mataifa duniani WHO limesema mwaka 2022 umegubikwa na changamoto lukuki za kiafya , kuanzia janga la COVID-19, Ebola, Mpoxy hadi vita vilivyokatili na kujeruhi wengi hata hivypo linasema kuna matumaini kwa mwaka ujao, yapi?

Taarifa ya tathmini ya kiafya ulimwenguni iliyotolewa leo na WHO nchini Geneva Uswisi imeeleza mwaka 2022, umeendelea kushuhudia uwepo wa janga la COVID-19 pamoja na mlipuko wa ugonjwa wa Mpox hapo awali ikifahamika kama Monkeypox ambao ulienea kwa kasi katika nchi mbalimbali duniani.

Sauti
2'24"
© UNICEF/Uganda

UNICEF yawezesha wanafunzi waliokuwa karantini Uganda kufanya mitihani

Nchini Uganda shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limewezesha wanafunzi wa shule moja ya msingi nchini humo kufanya mtihani wa kuhitimu shule ya msingi baada ya shule hiyo kulazimika kufungwa na wanafunzi kuwekwa karantini kufuatia mwanafunzi mmoja kupata maambukizi ya Ebola, mlipuko uliotangazwa mwezi SEptemba mwaka huu.

Tarehe 20 mwezi Septemba mwaka huu wa 2022, Wizara  ya Afya nchini Uganda ilitangaza mlipuko wa Ebola, mlipuko ambao ulihatarisha kuvuruga mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi kwa wanafunzi wa darasa la saba. 

Sauti
2'6"