Wakati hivi karibuni kumeibuka aina mpya ya virusi vya corona au COVID-19 barani Afrika ambavyo kiwango cha maambukizi yake ni cha juu zaidi, shirika la afya duniani WHO leo limetoa wito kwa nchi zote za bara hilo kuongeza kiwango cha ufuatiliaji na tathimini kupitia mtandao wa maabara Afrika ili kubaini mwenendo wowote mpya wa maambukizi na kuimarisha juhudi za kukabiliana na mlipuko huo.